Translate

Friday, May 23, 2014

JAMANI TANZANIAA DA HATA SITO HAMA NAKUPENDA TANZANIA


Jozani Forest - Zanzibar
 Ukiwa unapenda wanyama pori basi hata kama utaenda visiwani utatamani uwaone hata kama ni wadogo na wachache. Visiwa vya Zanzibar, vimejaaliwa kuwa na aina ya pekee ya mbega ambao wanapatokana Visiwani humo tu. Hao ni Zanzibar Red colobus monkeys - Mbega wekundu wa Zanzibar. Na msitu wa Jozani ndio eneo mahususi lililotengwa kuwahifadhi na kuwapa fursa wengine kuja kuwaona viumbe hawa adimu. Tofauti na misitu na hifadhi nyingi za Hapa nchini, Msitu wa Jozani mgeni hutembea kwa miguu kuwasaka Mbega walipo. inategemea na muda na hali ya mazingira kwani unaweza tembea kwa masaa kadhaa ili kuwapata. Siku hii ilituchukua muda mfupi sana kuwaona kwani ilikuwa ni mida ya jioni na walikuwa wamesogea karibu kabisa na geti la kuingilia kwenye hifadhi.

No comments:

Post a Comment

ADD COMMENTS