JAMANI TANZANIAA DA HATA SITO HAMA NAKUPENDA TANZANIA
Ukiwa unapenda wanyama pori basi hata kama utaenda visiwani utatamani
uwaone hata kama ni wadogo na wachache. Visiwa vya Zanzibar, vimejaaliwa
kuwa na aina ya pekee ya mbega ambao wanapatokana Visiwani humo tu. Hao
ni Zanzibar Red colobus monkeys - Mbega wekundu wa Zanzibar. Na msitu
wa Jozani ndio eneo mahususi lililotengwa kuwahifadhi na kuwapa fursa
wengine kuja kuwaona viumbe hawa adimu. Tofauti na misitu na hifadhi
nyingi za Hapa nchini, Msitu wa Jozani mgeni hutembea kwa miguu kuwasaka
Mbega walipo. inategemea na muda na hali ya mazingira kwani unaweza
tembea kwa masaa kadhaa ili kuwapata. Siku hii ilituchukua muda mfupi
sana kuwaona kwani ilikuwa ni mida ya jioni na walikuwa wamesogea karibu
kabisa na geti la kuingilia kwenye hifadhi.
No comments:
Post a Comment
ADD COMMENTS