Translate

Saturday, March 1, 2014

Samuel Eto'o alichukizwa na kejeli ya Mourinho kuhusu umri wake, amjibu kwa kejeli pia.

urday, March 01, 2014

Mshambuliaji wa Chelese, Samuel Eto’o amechukizwa na kauli iliyotolewa na kocha wake Jose Mounrinho, kauli iliyoonekana kukeje umri wa mshambuliaji huyo kuwa sehemu ya kikwazo cha timu yake kupata ushindi dhidi ya Galatasaray.

Kipande cha video kinachoonesha maongezi ya Mourinho kilirushwa na Canal Plus, ambapo ilikuwa ni sehemu ya maongezi faragha kati yake na mfanyabiashara mmoja.
“Tatizo la Chelsea ni kwamba nakosa mfungaji. Eto’o ana miaka 32, labda 35, nani anajua?” alisema Mounrinho.
Hata hivyo Samuel Eto’o ambaye ana umri wa miaka 32, alijibu pia kwa kejeli kwa kutumia takwimu ile ile aliyoitoa Mourinho, na kudai kuwa kama aliweza kufunga magoli matatu dhidi ya Manchester akiwa na miaka 37 basi anaweza kufunga magoli mengi zaidi hata akiwa na miaka 50.
Baada ya maelezo ya Mourinho kuoneshwa kwenye television, kocha huyo aliomba radhi na kueleza kuwa bado uhusiano wake na Eto’o haukuathiriwa na tukio hilo.
Naye Caude Le Roy aliyewahi kufanya kazi na timu ya taifa ya Cameroon alieleza kuwa aliongea na Eto’o kwa njia ya simu na kwamba alionesha kukasirishwa na kauli ya Mourinho.

No comments:

Post a Comment

ADD COMMENTS